Hatua ya kwanza ikiwa imebeba hatua zote kwani biashara inahitaji utayari (kuamua) zaidi ya vitu vingine kama mtaji nk
Hatua ya ya 1: Kuamua kuingia katika biashara
Kuamua kuingia katika biashara ni majumuisho ya utayari wa kisaikolojia, kiakili, kiuchumi na kukabiliana na hatari au vitisho vyote vitakavyojitokeza kwenye biashara
Maamuzi yako na hasa maamuzi magumu juu ya aidha kufanya hiyo biashara au la si ile hali ya kuamua kufanya biashara tu, bali pia ni ile hali ya kukubaliana na ups and downs za biashara husika na kuwa tayari kujitoa mhanga zaidi.
Hatua ya 2: Kuchanganua uwezo na udhaifu wako
Maeneo manne ni muhimu yapatiwe taarifa halisi na kuchukua hatua ili uweze kumudu kufanya biashara husika
Mazingira wezeshi Mazingira pingamizi
Mazingira ya Ndani UwezoUwezo wako katika kuendesha biashara mfano: utaalam, vitendea kazi, kiwanja nk. UdhaifuUdhaifu wako katika kuendesha biashara mfano: ukosefu wa utaalam, vitendea kazi, kiwanja nk.
Mazingira ya Nje FursaKuwepo kwa sera nzuri, katiba nzuri, hali ya hewa nzuri, mwitikio wa jamii nk VitishoKutokuwepo kwa sera nzuri, katiba nzuri, hali ya hewa nzuri, mwitikio mbaya wa jamii nk
Hatua ya 3: Kupata mafunzo
Baada ya kujua udhaifu wako, pata mafunzo
Mfano:- Ya kupata ufundi au kubadili mitizamo
Kupata utaalam wa kiufundi katika biashara husika
Hatua ya 4: Kupeleleza mazingira utakayofanya biashara
No comments:
Post a Comment